Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 5 Sitting 4 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Waziri wa Mifugo na Uvuvi 43 2021-11-05

Name

Dr. Stephen Lemomo Kiruswa Mamasita

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Longido

Primary Question

MHE. DKT. STEVEN L. KIRUSWA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itaboresha Miundombinu ya Minada ya Mifugo kwa kujenga mazizi ya kisasa, vyoo na ofisi za kupokea tozo na kodi za mnada?

Name

Abdallah Hamis Ulega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkuranga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Mifugo na Uvuvi naomba kujibu swali la Mheshimiwa Steven Lemomo Kiruswa - Mbunge wa Longido kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali imeendelea kuboresha minada nchini ambapo katika mwaka wa fedha 2021/2022 Wizara katika bajeti ya maendeleo imetenga kiasi cha Shilingi Bilioni 4.46 kwa ajili ya kukarabati na kujenga miundombinu ya minada 19 ya upili mpakani na ya awali kwa kujenga uzio, ofisi, mazizi ya kisasa ya ng’ombe na mbuzi, vyoo, vipakilio na mabirika ya kunywea maji mifugo katika minada ya Pugu (Dar es Salaam), Mkiu (Pwani), Mtukula (Kagera), Horohoro (Tanga), Ndelema (Tanga), Malampaka (Simiyu), Magena (Mara), Igunga-(Tabora), Buhigwe (Kigoma), Ipuli (Tabora), Wasso (Arusha), Gendi (Manyara), Kileo (Kilimanjaro), Meserani (Arusha), Nyanguge (Mwanza), na Nyamatala (Mwanza). Utekelezaji unatarajiwa kuanza mwezi huu wa Novemba, 2021 na utachukua miezi minne kukamilika.

Mheshimiwa Spika, Serikali itaendelea kuboresha miundombinu ya minada nchini kulingana na uwezo wa kibajeti. Ahsante.