Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 3 Sitting 53 Energy and Minerals Wizara ya Nishat 457 2016-06-29

Name

Lolesia Jeremia Maselle Bukwimba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Busanda

Primary Question

MHE. LOLESIA J. BUKWIMBA aliuliza:-
Je, ni lini Serikali itawapa maeneo ya uchimbaji wachimbaji wadogo wa Kata za Nyarugusu, Nyaruyeye na Kaseme?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nishati na Madini, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Lolesia Jeremiah Bukwimba, Mbunge wa Busanda kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, mwaka 2001 Wizara ilitenga eneo lenye ukubwa wa hekta 533.55 kwa ajili ya wachimbaji wadogo katika eneo la Nyarugusu. Pamoja na hatua hiyo, wachimbaji wadogo wameendelea kuomba kumilikishwa maeneo hasa ya Buziba yanayomilikishwa na Kampuni ya Buckreef Gold Ltd, kupitia leseni namba PL 6545/2010. Leseni hii itaisha muda wake tarehe 11 Julai, 2016.
Mheshimiwa Naibu Spika, maeneo ya Nyaruyeye na Kaseme pia yana leseni hai ya utafutaji wa madini yenye leseni RL 0007/2012 ya Kampuni ya ARL ambayo pia itaisha muda wake tarehe 20 Septemba, 2017. Kwa sasa Serikali inafanya mazungumzo na kampuni hizo ili kuona uwezekano wa kuachia maeneo kwa ajili ya wachimbaji wadogo.
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali itaendelea na utaratibu wa kutenga maeneo kwa ajili ya shughuli za wachimbaji wadogo hapa nchini. Wakala wa Jiolojia Tanzania (GST) wanaendelea kutathmini maeneo mbalimbali ili kuona kama maeneo hayo yana mashapo ya kutosha kwa ajili ya wachimbaji wadogo.
Aidha, Serikali itaendelea kujadiliana na kampuni zinazomiliki leseni za madini kwa wachimbaji hapa nchini kwa ajili ya kuwagawia wachimbaji wa maeneo ya Nyarugusu, Nyaruyeye pamoja na Kaseme.
Mheshimiwa Naibu Spika, hata hivyo, katika kutenga maeneo kwa ajili ya wachimbaji wadogo, vigezo vinavyozingatiwa ni pamoja na uwepo wa eneo lililo wazi kwa ajili ya kuwagawia wachimbaji kwa mujibu wa Sheria ya Madini ya mwaka 2010.