Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 5 Sitting 3 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Waziri wa Mifugo na Uvuvi 36 2021-11-04

Name

Angelina Adam Malembeka

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ANGELINA ADAM MALEMBEKA aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kuanzisha Benki ya Wavuvi nchini?

Name

Abdallah Hamis Ulega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkuranga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Mifugo na Uvuvi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Angelina Adam Malembeka, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kumjulisha Mheshimiwa Mbunge kwamba Benki ya Maendeleo ya Kilimo (TADB) tayari ipo kwa ajili ya kutoa huduma za kifedha kwa wadau wa sekta za kilimo, mifugo na uvuvi. Benki hii ilianzishwa mnamo mwezi Septemba, 2012 chini ya Sheria ya Makampuni (Sura ya 212).

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali ilianzisha Benki hiyo ili kusaidia kuongoza mageuzi ya kuleta maendeleo kwenye sekta ya kilimo sambamba na kujenga uwezo wa wadau kutekeleza programu mbalimbali za kuongeza thamani mazao ya kilimo, mifugo na uvuvi. Benki hii inatoa mikopo ya muda mfupi, wa kati na mrefu kwa watu binafsi na vikundi vinavyojishughulisha na sekta ya kilimo, mifugo na uvuvi.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kumshauri Mheshimiwa Mbunge awahamasishe wavuvi kuchangamkia fursa mbalimbali za mikopo na huduma nyinginezo za kifedha zinazotolewa na Benki ya Maendeleo ya Kilimo. Ahsante.