Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 5 Sitting 3 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 32 2021-11-04

Name

Selemani Jumanne Zedi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukene

Primary Question

MHE. SELEMANI J. ZEDI aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itajenga Jengo la Wodi za kulaza Wagonjwa pamoja na kupeleka mashine ya X-ray katika Kituo cha Afya Itobo kilichopo Jimbo la Bukene?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Selemani Jumanne Zedi, Mbunge wa Jimbo la Bukene, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, katika mwaka wa fedha 2021/2022, Serikali imepeleka shilingi milioni 250 katika Kata ya Itobo kwa ajili ya ujenzi wa majengo ya kituo hicho ili kiweze kuwa na uwezo wa kutoa huduma za upasuaji. Ujenzi wa majengo hayo umeanza na unatarajiwa kukamilika ifikapo 30 Aprili, 2022.

Mheshimiwa Naibu Spika, ujenzi wa vituo hivi vya afya unafanyika kwa awamu. Hivyo, baada ya awamu hii ya kwanza ya ujenzi kukamilika, Serikali itaendelea kutafuta fedha kwa ajili ya ujenzi wa majengo mengine ikiwemo wodi katika Kituo cha Afya cha Itobo. Aidha, mashine za X-ray zitaendelea kununuliwa kadri ya upatikanaji wa fedha. Ahsante.