Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 5 Sitting 2 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Waziri wa Mifugo na Uvuvi 29 2021-11-03

Name

Vincent Paul Mbogo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkasi Kusini

Primary Question

MHE. VINCENT P. MBOGO aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itajenga masoko ya samaki katika Ukanda wa Ziwa Tanganyika hususani Kata ya Kala Mpasa, Wampambe, Kizimbi na Naninde ili wavuvi wapate maeneo ya kuuzia samaki badala ya kulazimika kwenda kuuza nchi za jirani za Zambia, Congo na Burundi?

Name

Abdallah Hamis Ulega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkuranga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Mifugo na Uvuvi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Vincent Paul Mbogo, Mbunge wa Nkasi Kusini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali inaendelea kujenga miundombinu ya uvuvi katika maeneo mbalimbali ikiwemo katika mwambao wa Ziwa Tanganyika. Miundombinu ya Mialo na Masoko ni muhimu katika kuhakikisha kuwa na mazao bora na salama, kupunguza upotevu wa mazao na kusaidia ukusanyaji wa taarifa na mapato ya Serikali.

Mheshimiwa Spika, pamoja na umuhimu huu, ujenzi wa masoko unahitaji rasilimali ikiwemo ardhi na fedha. Napenda kumhakikishia Mheshimiwa Mbunge kuwa Serikali ipo tayari kujenga Soko, katika Wilaya ya Nkasi kwa kuzingatia upatikanaji wa fedha.

Mheshimiwa Spika, namuomba Mheshimiwa Mbunge kwa kushirikiana na Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi kuandaa eneo katika Wilaya ya Nkasi, ili kuwezesha hatua za ujenzi wa soko kuanza pindi fedha itakapopatikana. Ahsante.