Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 5 Sitting 2 Education, Science,Technology and Vocational Training, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia 28 2021-11-03

Name

Mussa Ramadhani Sima

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Mjini

Primary Question

MHE. MUSSA R. SIMA aliuliza: -

Je, Serikali haioni haja ya kulifanya somo la kilimo kuwa la lazima kuanzia ngazi ya elimu msingi mpaka chuo kikuu kwa kuwa kilimo ni uti wa mgongo wa uchumi?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Sayansi na Teknolojia, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mussa Ramadhani Sima, Mbunge wa Singida Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua umuhimu na mchango mkubwa wa Kilimo katika maendeleo ya familia na taifa kwa ujumla.

Mheshimiwa Spika, somo la kilimo linafundishwa katika ngazi zote za elimu hapa nchini. Kwa mfano, katika ngazi ya mtaala wa ngazi ya elimu ya msingi maarifa na stadi za kilimo zinafundishwa katika somo la stadi za kazi. Kwa upande wa Sekondari, somo la kilimo ni somo chaguzi na linasomwa na wanafunzi kuanzia kidato cha Kwanza hadi cha Sita.

Mheshimiwa Spika, Serikali pia inahuisha miongozo ya eimu ya kujitegemea kuanzia shule za msingi hadi vyuo vya ualimu. Miongozo hiyo imelenga kuziwezesha shule na vyuo vya ualimu kuanzisha na kusimamia kwa ufanisi miradi ya uzalishaji mali ikiwemo shughuli za kilimo na biashara. Elimu hiyo itamsaidia mwanafunzi kujifunza kwa vitendo stadi mbalimbali za maisha ikiwa ni pamoja na kilimo kwa lengo la kuwajengea misingi imara ya kujitegemea na kujiajiri.

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa sasa Wizara kupitia Taasisi ya Elimu Tanzania inafanya mapitio ya mitaala ya ngazi zote za elimu msingi, suala hili litajadiliwa na kufanyiwa maamuzi stahiki. Ahsante.