Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 5 Sitting 2 Education, Science,Technology and Vocational Training, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia 27 2021-11-03

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Primary Question

MHE. JUMANNE A. SAGINI aliuliza: -

Je, lini Serikali itaanza rasmi ujenzi wa Chuo Kikuu cha Mwalimu Julius K. Nyerere cha Teknolojia na Kilimo, Butiama?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, naomba sasa kujibu swali la Mheshimiwa Jumanne Abdallah Sagini Mbunge wa Butiama kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali imeshaanza mchakato wa kukijenga Chuo Kikuu cha Teknolojia ya Kilimo cha Mwalimu Nyerere, Kampasi ya Butiama. Katika kutimiza azma hiyo, Serikali imetenga Dola za Kimarekani Millioni 44.5, sawa na Shilingi za Kitanzania Bilioni 103 kupitia mradi wa Mageuzi ya Kiuchumi kwa ajili ya Elimu ya Juu uitwao Higher Education for Economic Transformation-HEET. Mradi wa HEET unatekelezwa kupitia Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia ikishirikiana na Benki ya Dunia kuanzia mwaka huu 2021 mwezi Septemba.

Mheshimiwa Spika, yapo baadhi ya maandalizi muhimu yaliyokamilika ambayo ni pamoja na: kupatikana kwa hati miliki ya eneo lenye ukubwa wa ekari 573.5; uandaaji wa mpango kabambe (master plan); tathmini ya athari ya mazingira (Environmental and Social Impact Assessment); na usanifu wa majengo.

Mheshimiwa Spika, kwa sasa taratibu zinazofuata ni kumtafuta mshauri mwelekezi, na atakapopatikana atafanya kazi ya mapitio ya michoro na kuandaa hadidu za rejea na makabrasha ya zabuni ili kutangaza na kumpata mkandarasi. Michakato hiyo itakapokamilika ujenzi huo utaanza rasmi.

Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana.