Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 5 Sitting 2 Public Service Management Ofisi ya Rais (Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora) 19 2021-11-03

Name

Saashisha Elinikyo Mafuwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Hai

Primary Question

MHE. SAASHISHA E. MAFUWE aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itabadilisha Muundo wa Utumishi wa Maafisa Utumishi/Utawala na Walimu ili waweze kuanza na Daraja E kama ilivyo Kada ya Sheria na nyinginezo?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Saashisha Elinkyo Mafuwe, Mbunge wa Jimbo la Hai, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Miundo ya Maendeleo ya Utumishi ya Kada mbalimbali inayotumika sasa katika Utumishi wa Umma iliandaliwa kwa kuzingatia matokeo ya zoezi la Tathmini ya Kazi iliyofanyika kuanzia mwaka 1998 hadi 2000. Aidha, Miundo husika ilianza kutekelezwa mwezi Julai, 2003.

Mheshimiwa Spika, matokeo ya zoezi la tathmini ya kazi iliyoainisha uzito wa majukumu ya kada mbalimbali katika utumishi wa umma na yaliyotumika kama msingi wa kupanga vianza mshahara kwa watumishi wa umma wa kada mbalimbali wakiwemo Maafisa Utumishi na Utawala ambao wanaanza na ngazi ya mishahara ya TGS D, walimu Daraja C yaani walimu wenye shahada ambao wanaanza na ngazi ya mshahara TGTS D na Maafisa Sheria ambao wanaanza na ngazi ya mshahara ya TGS E.

Mheshimiwa Spika, mwaka 2015 hadi 2017 Serikali iliendesha zoezi lingine la tathmini ya Kazi katika Utumishi wa Umma ambalo lililenga kubaini uzito wa majukumu kwa kada mbalimbali. Katika kuoanisha na kuwianisha viwango vya mishahara vya watumishi katika Utumishi wa Umma, Serikali itatumia matokeo ya mapendekezo ya zoezi hilo kupanga vianzia mshahara vya kada mbalimbali ikiwa ni pamoja na Maafisa Utumishi na Utawala na Walimu kwa kuzingatia uwezo wa kibajeti. Naomba kuwasilisha.