Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 5 Sitting 1 Finance and Planning Wizara ya Fedha na Mipango 14 2021-11-02

Name

Jafari Chege Wambura

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Rorya

Primary Question

MHE. JAFARI W. CHEGE aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itaboresha mpaka wa Kirongwe kwa kujenga One Border Post ili kuimarisha na kuongeza mapato ya Serikali?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Fedha na Mipango, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Jafari Wambura Chege, Mbunge wa Rorya kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali ina mpango wa kuboresha mpaka wa Kirongwe kwa kuweka miundombinu wezeshi itakayotoa kutoa huduma kwa pamoja. Aidha, katika mwaka 2021/2022, Serikali imetenga fedha kiasi cha shilingi million 407 kwa ajili ya usanifu na ujenzi wa nyumba za makazi za watumishi Kirongwe. Vilevile, katika mwaka 2022/2023 Serikali imepanga kuboresha mipaka mbalimbali nchini ikiwemo mpaka wa Kirongwe ili taasisi za Serikali ziweze kutoa huduma kwa pamoja.

Mheshimiwa Spika, Serikali itaendelea kuimarisha mipaka yetu kwa kujenga nyumba za makazi kwa watumishi wa taasisi zinazofanya kazi mipakani na ofisi za kutolea huduma kwa pamoja mipakani ili kuboresha ulinzi na usalama wa nchi na pia kuongeza mapato ya Serikali.