Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 5 Sitting 1 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 10 2021-11-02

Name

Ravia Idarus Faina

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Makunduchi

Primary Question

MHE. RAVIA IDARUS FAINA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itajenga Ofisi za NIDA katika Wilaya ya Kusini Unguja?

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Ravia Idarus Faina, Mbunge wa Jimbo la Makunduchi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua umuhimu wa kuwa na Ofisi za Wilaya kwa ajili ya kuwafikishia wananchi huduma za usajili na utambuzi wa vitambulisho karibu na maeneo yao. Katika kutekeleza mpango huo, Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) imefanikiwa kufungua ofisi 150 katika Wilaya zote za Tanzania Bara na Visiwani.

Mheshimiwa Spika, Ofisi ya NIDA katika Wilaya ya Kusini, Mkoa wa Kusini Unguja itajengwa katika Mwaka wa Fedha 2022/2023. Nakushukuru.