Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 5 Sitting 1 Water and Irrigation Wizara ya Maji 5 2021-11-02

Name

Dunstan Luka Kitandula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkinga

Primary Question

MHE. JOHN M. SALLU K.n.y. MHE. DUNSTAN L. KITANDULA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi ya kuvipatia maji kutoka mradi wa Mapatano Vijiji vya Kwangena, Bantu na Machimboni Wilayani Mkinga?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maji naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dunstan Luka Kitandula Mbunge wa Jimbo la Mkinga kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, jukumu la Serikali ni kuhakikisha maeneo yote ya vijijini huduma ya upatikanaji wa maji inaboreshwa. Ambapo katika mwaka wa fedha 2021/2022 kazi ya upanuzi wa skimu ya maji ya Mapatano inafanyika. Ili kufikisha maji katika vijiji vya Kwangena, Bantu na Machimboni ambavyo mahitaji ya maji ni lita 251,000 kwa siku.

Mheshimiwa Spika, katika upanuzi huo kazi zitakazofanyika ni kulaza mabomba Kilomita 29 na kujenga matenki mawili (2) ya kuhifadhi maji lita 45,000 na lita 135,000. Kazi hii inatarajiwa kukamilika mwezi Agosti, 2022 na utanufaisha wananchi takriban 11,000.