Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 5 Sitting 1 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Waziri wa Mifugo na Uvuvi 4 2021-11-02

Name

Norah Waziri Mzeru

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NORA W. MZERU aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kuwasaidia wafugaji wa Mkoa wa Morogoro kufanya ufugaji wa kisasa na wenye tija kwa kuwa Mkoa huu una wafugaji wengi?

Name

Abdallah Hamis Ulega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkuranga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Mifugo na Uvuvi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Nora Waziri Mzeru Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Wizara imekuwa ikifanya jitihada mbalimbali, ili kufanya ufugaji katika Mkoa wa Morogoro kuwa wenye tija na wa kisasa. Juhudi hizo ni pamoja na uboreshaji wa mbari za mifugo kwa kuhimilisha ngómbe, kuwezesha upatikanaji wa kuku wazazi walioboreshwa, mafunzo rejea juu ya teknolojia za ufugaji bora kwa wafugaji na maafisa ugani. Vipindi vya elimu kwa umma vya redio, televisheni, maonyesho mbalimbali yakiwemo ya sabasaba na nanenane.

Mheshimiwa Spika, kutokana na juhudi hizi, hadi mwaka 2020 mifugo iliyoboreshwa katika Mkoa wa Morogoro imefikia ng’ombe 28,582 sawa na asilimia 3 ya ng’ombe wote na mbuzi 19,899 sawa na asilimia 11 ya mbuzi wote na kuku millioni 2.5 sawa na asilimia 69 ya kuku wote.

Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2021/2022 Wizara kwa kushirikiana na wadau na Mamlaka za Serikali za Mitaa, inatarajia kuhimilisha ng’ombe 32,606 Mkoani Morogoro, kwa kutumia mbegu bora za mifugo za ruzuku kutoka katika Kituo cha Taifa cha Uhimilishaji cha NAIC Arusha. Ahsante sana.