Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 5 Sitting 1 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 3 2021-11-02

Name

Nancy Hassan Nyalusi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NANCY H. NYALUSI aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itaanza na kukamilisha ujenzi wa barabara ya Igowole – Nyigo kilomita 54 ambayo imetajwa kwenye Ilani ya Chama cha Mapinduzi ya mwaka 2020 – 2025?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. MWITA M. WAITARA) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi naomba kujibu swali la Mheshimiwa Nancy Hassan Nyalusi, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, barabara anayoizungumzia Mheshimiwa Mbunge ni barabara ya Mkoa ya Igowole - Kasanga – Nyigo yenye urefu wa kilometa 54.51, inayosimamiwa na Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi sekta ya Ujenzi kupitia Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS).

Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua umuhimu wa barabara ya Igowole – Kasanga – Nyigo yenye urefu wa kilomita 54.51 kwa Wananchi wa Wilaya ya Mafinga. Kwa sasa, Serikali inaendelea kutafuta fedha kwa ajili ya kuifanyia upembuzi yakinifu na usanifu wa kina na hatimaye kujengwa kwa kiwango cha lami.

Mheshimiwa Spika, wakati Serikali ikiendelea na juhudi za kutafuta fedha ili kujenga barabara hii kwa kiwango cha lami, Wizara yangu kupitia TANROADS inaendelea kuifanyia matengenezo mbalimbali barabara hii, ili iendelee kupitika majira yote ya mwaka. Katika mwaka wa fedha 2021/2022 kiasi cha shilingi milioni 66 kimetengwa kwa ajili ya kazi hiyo. Ahsante.