Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 5 Sitting 1 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 1 2021-11-02

Name

Issa Jumanne Mtemvu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibamba

Primary Question

MHE. ISSA J. MTEMVU aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango wa kujenga kwa kiwango cha lami barabara za Mbezi Shule – Mpiji Magohe – Bunju kupitia Mabwe Pande na Kibamba Njia Panda – Mpiji Magohe kama zilivyoainishwa kwenye Ilani ya CCM ya mwaka 2020 - 2025?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, ninapenda kujibu swali la Mheshimiwa Issa J. Mtemvu, Mbunge wa Kibamba kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, barabara ya Mbezi Shule – Mpiji Magohe – Bunju kupitia Mabwe Pande ni barabara inayotambulika kwa jina la Mbezi Victoria – Mpiji Magohe hadi Bunju yenye urefu wa kilometa 25; na barabara ya Kibamba Njia Panda – Mpiji Magohe inatambulika kwa jina la Kibamba Shule hadi Mpiji Magohe ambayo ina urefu wa kilometa 8.7.

Mheshimiwa Spika, barabara hizi ni sehemu ya barabara ya Mzunguko wa Nje wa jiji la Dar es Salaam (Outer Ring Roads) inayoanzia Bunju – Mpiji Magohe – Kibamba – Pugu Kajiungeni – Mzinga – Tuangoma mpaka Kigamboni ambayo ina urefu wa kilometa 61.

Mheshimiwa Spika, Serikali ipo katika mpango wa kujenga barabara hizi kwa kiwango cha lami. Katika Mwaka wa Fedha wa 2021/2022 jumla ya Shilingi milioni 600 zimetengwa kwa ajili ya kazi ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa barabara ya mzunguko wa nje inayoanzia Bunju – Mpiji Magohe – Kibamba – Pugu Kajiungeni – Mzinga – Tuangoma mpaka Kigamboni na mzunguko wa ndani inayoanzia – Mbezi Mwisho – Kifuru – Banana – Kipara hadi Kigamboni. Taratibu za kumpata Mhandisi Mshauri wakufanya kazi hiyo zipo katika hatua za mwisho za uchambuzi wa zabuni. Mara baada ya kazi hiyo kukamilika, Serikali itatafuta fedha kwa ajili ya ujenzi kwa kiwango cha lami. Ahsante.