Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 4 Sitting 9 Finance and Planning Wizara ya Fedha na Mipango 118 2021-09-10

Name

Priscus Jacob Tarimo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Moshi Mjini

Primary Question

MHE. PRISCUS J. TARIMO aliuliza: -

Je, ni nini hatma ya biashara ya maduka ya kubadilisha fedha (Bureau de Change) yaliyofungwa na Serikali?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Fedha na Mipango, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Priscus Jacob Tarimo, Mbunge wa Moshi Vijijini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ukaguzi ambao umefanyika mwaka 2018/2019 ulisababisha maduka mengi ya kubadilisha fedha za kigeni kufungwa kutokana na kubainika kuendesha biashara bila kuzingatia sheria na kanuni husika. Baada ya kufungwa kwa maduka hayo, benki za biashara nchini zilihamasishwa kuendelea kutoa huduma ya kubadilisha fedha za kigeni katika matawi yake yote nchini. Kwa sasa benki zote za biashara zinatoa huduma hizo nchi nzima.

Mheshimiwa Spika, pia maduka ambayo hayakufungwa yameendelea kufungua matawi na kutoa huduma hizo katika miji mbalimbali nchini. Kwa ujumla hali ya upatikanaji wa huduma ya kubadilisha fedha za kigeni nchini ni ya kuridhisha. Aidha, maduka yaliyofungwa pamoja na kampuni nyingi ambayo yanayotaka kufanya biashara ya kubadilisha fedha za kigeni nchini, yanaruhusiwa kuomba leseni Benki Kuu kwa kuzingatia matakwa ya Sheria za Fedha za Kigeni ya mwaka 1992 pamoja na Kanuni za Biashara ya Kubadilisha Fedha za Kigeni ya mwaka 2019. Hadi kufikia tarehe 30 Julai 2021, Benki Kuu ilikuwa imepokea maombi mapya manne ya leseni ya biashara ya kubadilisha fedha za kigeni ambazo yanafanyiwa uchambuzi na wahusika watapewa leseni iwapo watakuwa wamekidhi vigezo.