Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 4 Sitting 9 Industries and Trade Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara 117 2021-09-10

Name

Zaytun Seif Swai

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ZAYTUN S. SWAI aliuliza: -

Je, ni lini akina Mama zaidi ya 300 waliokuwa Wafanyakazi wa Kiwanda cha Kiliflora Wilayani Meru watalipwa stahiki zao baada ya Kiwanda hicho kufungwa?

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Viwanda na Biashara, naomba kujibu swali la Zaytun Seif Swai, Mbunge Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua mgogoro uliopo baina ya wafanyakazi na mwekezaji wa Kampuni ya Kiliflora Ltd. Hivyo, Serikali ilifuatilia mgogoro huo na kubaini kuwa Tanzania Investment Bank (TIB) ilirejesha fedha iliyokopesha kwa kuuza mali za Kiliflora Ltd zilizowekwa dhamana ili kulipa deni la mkopo uliochukuliwa na Kampuni. Hivyo, kisheria Wafanyakazi wanapaswa kulipwa na Kampuni ya Kiliflora kwa kuwa kilichofanyika ni ufilisi kabidhi na siyo kufunga kampuni. Mfilisi Kabidhi (Receiver and Manager) ni tofauti na Mfunga Kampuni (Liquidator).

Mheshimiwa Spika, aidha, wafanyakazi wa Kiliflora Ltd, Wilson Samwel na Wenzake 502 walifungua Kesi ya Labor Na. ARS/ARM/305/2020, 152/2020 dhidi ya Kampuni ya Kiliflora Ltd na Frank Mwalongo ambaye ni Mfilisi Kabidhi ambayo ilianza kusikilizwa tarehe 30/10/2020. Shauri hili lilikwishatolewa maamuzi na Mahakama kwamba, masuala ya madai ya wafanyakazi yanapaswa kufanyiwa kazi na Kampuni ya Kiliflora Ltd maana haijafilisiwa kama ilivyoonekana kwenye taarifa za BRELA kwamba, Kampuni bado ipo hai.

Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Wizara ya Fedha na Mipango inaendelea kuhimiza mmiliki wa shamba la Kiliflora kuwalipa akina mama hao. Nakushukuru.