Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 4 Sitting 9 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 115 2021-09-10

Name

Issa Ally Mchungahela

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lulindi

Primary Question

MHE. ISSA A. MCHUNGAHELA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itaweka Kituo cha Uhamiaji katika eneo la Chipingo ili kuondokana na vivuko bubu vilivyopo Mpakani mwa Tanzania na Msumbiji?

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Issa Ally Mchungahela, Mbunge wa Lulindi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Chipingo ni kipenyo kilichopo Wilaya ya Masasi katika mpaka wa Tanzania na Msumbiji kandokando ya Mto Ruvuma umbali wa Kilomita 86 kutoka Masasi Mjini. Kwa upande wa Msumbiji hakuna ofisi za Uhamiaji wala huduma za Uhamiaji bali kuna walinzi wa mpaka wa nchi hiyo.

Mheshimiwa Spika, ufunguaji wa vituo vya mipakani hutegemea makubaliano baina ya nchi zinazochangia mpaka. Kwa upande wa mpaka wa Tanzania na Msumbiji, kumebaki kituo kimoja cha mpakani kinachofanya kazi cha Mtambaswala kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo ghasia na hali tete ya usalama.

Mheshimiwa Spika, kwa kuzingatia maelezo hayo, Serikali inaendelea kufuatilia hali ya usalama katika mpaka huo na hali itakapotengemaa mawasiliano na Msumbiji yatafanyika ili kufungua vituo zaidi kuhudumia wananchi wanaotumia mpaka huo. Ninakushukuru.