Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 4 Sitting 9 Health and Social Welfare Wizari wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto 110 2021-09-10

Name

Josephine Johnson Genzabuke

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE aliuliza: -

Je, ni kwa kiasi gani Serikali imewezesha Maafisa Maendeleo ya Jamii ambao wamepewa jukumu kubwa la kuanzisha na kusimamia shughuli za vikundi vya Maendeleo kwenye Halmashauri ili waweze kutimiza majukumu yao ipasavyo?

Name

Mwanaidi Ali Khamis

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO (MHE. MWANAIDI ALI KHAMISI) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Josephine Johnson Genzabuke, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali inawezesha Maafisa Maendeleo ya Jamii kupata vitendeakazi kadri Bajeti inavyoruhusu, ambapo hadi sasa imewapatia pikipiki 29 Maafisa wa Maendeleo ya Jamii wa Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino Mkoani Dodoma na Halmashauri ya Wilaya ya Tanganyika Mkoani Katavi.

Mheshimiwa Spika, aidha, Serikali kupitia Ofisi ya Rais, TAMISEMI imetoa kanuni za utoaji na usimamizi wa mikopo kwa vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu, marekebisho haya ya mwaka 2021. Kupitia kanuni hii, Maafisa hawa hutengewa fedha kutoka kwenye marejesho kwa ajili ya ufuatiliaji wa mikopo hiyo.

Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba kuwasilisha. (Makofi)