Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 4 Sitting 8 Natural Resources and Tourism Wizara ya Maliasili na Utalii 104 2021-09-09

Name

Innocent Edward Kalogeris

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Morogoro Kusini

Primary Question

MHE. INNOCENT E. KALOGERIS aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kuvuna mamba katika Mto Ruvu hasa katika Vijiji vya Kigamila, Bwila juu, Magogoni, Bwila chini, Kongwa, Tulo, Lukuhinge, Kata za Mvuha na Serembala katika Halmashauri ya Morogoro Vijijini, ili kupunguza vifo vinavyosababishwa na mamba hao?

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Innocent Edward Kalogeris, Mbunge wa Morogoro Kusini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inaendelea kufanya tathmini ya mamba katika mito iliyopo katika Mikoa ya Katavi, Rukwa na Morogoro. Baada ya tathmini hiyo kukamilika na kubainika kuwa idadi ya mamba waliopo ni kubwa, mamba hao watavunwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, aidha, endapo itabainika kuwa idadi ya mamba katika maeneo husika ni ndogo, Serikali itabaini mamba wanaosababisha adha kwa wananchi na kuwavuna ili wasiendelee kuleta madhara makubwa kwa wananchi. Naomba kuwasilisha. (Makofi)