Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 4 Sitting 8 Energy and Minerals Wizara ya Nishat 103 2021-09-09

Name

Flatei Gregory Massay

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Vijijini

Primary Question

MHE. FLATEI G. MASSAY aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itapeleka Mradi wa Ujazilizi katika Mkoa wa Manyara na Jimbo la Mbulu Vijijini ili kuwafikia wananchi wengi ambao hawakupitiwa na Mradi wa REA I, II na III?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Nishati, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Flatei Gregory Massay Mbunge wa Mbulu Vijijini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) inaendelea na utekelezaji wa miradi ya ujazilizi kupitia mpango wa kupeleka umeme vijijini, ili kufikisha umeme katika vitongoji vya Tanzania Bara vikiwemo vitongoji vya Jimbo la Mbulu Vijijini. Miradi hii inatekelezwa awamu kwa awamu kulingana na upatikanaji wa fedha.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika kipindi cha Mwaka 2021/2022, jumla ya vitongoji 246 katika Mkoa wa Manyara vikiwemo vitongoji vyote visivyo na umeme katika Jimbo la Mbulu Vijijini vinatarajiwa kufikishiwa umeme. Gharama ya Mradi ni shilingi bilioni 45. Zoezi la kupeleka umeme katika vitongoji ni endelevu linalotekelezwa kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) pamoja na TANESCO.