Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 4 Sitting 7 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 91 2021-09-08

Name

Catherine Valentine Magige

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. CATHERINE V. MAGIGE aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itamlipa Mkandarasi anayetengeneza kwa kiwango cha lami barabara ya kutoka Loliondo hadi Mto wa Mbu ili iweze kukamilika na kurahisisha maisha ya Wakazi wa Ngorongoro?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. MWITA M. WAITARA) alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi napenda kujibu swali la Mheshimiwa Catherine Valentine Magige, Mbunge Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Ujenzi wa barabara ya Loliondo – Mto wa Mbu sehemu ya Wasso – Sale yenye kilometa 49 ulianza Oktoba, 2017 ambapo hadi kufikia Julai, 2021 utekelezaji wa kazi ulikuwa umefika asilimia 83. Serikali inaendelea kumlipa Mkandarasi wa mradi huu pamoja na Makandarasi wa miradi mingine ya maendeleo inayoendelea hapa nchini kulingana na hati za madai zinazowasilishwa na kuhakikiwa na Wizara ya Fedha na Mipango. Hadi kufikia Juni, 2021, Mkandarasi wa ujenzi wa barabara hii amelipwa jumla ya shilingi bilioni 38.07. Ahsante.