Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 4 Sitting 7 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 83 2021-09-08

Name

Kassim Hassan Haji

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mwanakwerekwe

Primary Question

MHE. KASSIM HASSAN HAJI aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itakamilisha ujenzi wa Kituo cha Polisi Mwanakwerekwe ambacho kiliwekwa jiwe la msingi mwaka 2008 na Kiongozi wa Mbio za Mwenge?

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Kassim Hassan Haji, Mbunge wa wananchi wa Jimbo la Mwanakwerekwe kama ifuatavyo: -

Mheshimwa Naibu Spika, Mwanakwerekwe kuna Kituo cha Polisi cha Daraja ā€œCā€ ambacho kinatumika hadi sasa na kinafanya kazi kwa saa ishirini na nne, na eneo hilo lilitolewa na Serikali baada ya kuhamisha Idara ya Maonyesho Zanzibar.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini eneo la Magogoni Amani kwa Mabata ndiko kuna jengo la kituo kidogo cha polisi, ambacho kinajengwa kwa nguvu za wananchi na jiwe la msingi liliwekwa na Kiongozi wa Mbio za Mwenge mwaka 2008 na ujenzi wake umefikia kwenye hatua ya renta. Serikali kupitia Jeshi la Polisi inatafuta fedha ili kumalizia ujenzi wa kituo hicho kiweze kuhudumia wananchi.

Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru.