Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 4 Sitting 7 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 80 2021-09-08

Name

Juliana Daniel Shonza

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JULIANA D. SHONZA aliuliza: -

Je, ni lini jengo jipya la hospitali lililojengwa Tunduma litafunguliwa na kuanza kutoa huduma kwa wananchi?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE) alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-TAMISEMI naomba kujibu swali la Mheshimiwa Juliana Daniel Shonza Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inaendelea kuboresha huduma za afya nchini kwa kutoa fedha za ukarabati na ujenzi wa vituo vya kutolea huduma za afya. Serikali imeupatia Mkoa wa Songwe kiasi cha shilingi billion 14.8 kwa ajili ya ujenzi wa hospitali nne kwenye Halmashauri ya Mji wa Tunduma, Halmashauri ya Wilaya ya Songwe, Momba na Ileje.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imeeendelea na ujenzi wa Hospitali ya Halmashauri ya Mji Tunduma ambao mpaka kukamilika inakadiriwa kugharimu shilingi bilioni 9.5. Mradi huu unatekelezwa kwa awamu mbili, ambapo awamu ya kwanza utahusisha ujenzi wa jengo la wagonjwa wa nje (OPD) uliogharimu kiasi cha shilingi bilioni nne. Ujenzi wa jengo hilo la ghorofa moja upo kwenye hatua ya umaliziaji. Kuanzia Julai 2021 jengo hilo lilianza kutumika kutoa huduma ya wagonjwa wa nje na kliniki ya mama wajawazito na watoto.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika mwaka wa fedha 2021/2022 Serikali imetenga fedha shilingi bilioni 1.5 kwa ajili ya kuendelea na ujenzi wa Hospitali ya Halmashauri ya Tunduma. Ujenzio huo wa majengo yatakayohusishwa ni pamoja na jengo la maabara, jengo la mionzi, jengo la huduma za dharura, jengo la afya ya kinywa na meno, macho, upasuaji na utawala.