Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 62 Water and Irrigation Wizara ya Maji 528 2021-06-30

Name

Dr. Christine Gabriel Ishengoma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT CHRISTINE G. ISHENGOMA aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kuongeza vituo vya kuchotea maji katika Mji Mdogo wa Gairo?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Christine Gabriel Ishengoma, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, hali ya upatikanaji wa huduma ya maji kwa wananchi wa Mji wa Gairo kwa sasa ni wastani wa asilimia 75. Katika Mwaka wa Fedha 2020/2021 Serikali imeendelea kuboresha huduma ya maji kwa wananchi kwa kufanya upanuzi wa mtandao wa maji katika Mji wa Gairo ambapo kazi zilizofanyika ni pamoja na ulazaji wa mabomba ya kusambaza maji umbali wa kilometa nane na ujenzi wa vituo vya kuchotea maji vitano, hivyo vituo hivyo vya kuchotea maji kuongezeka kutoka vituo 70 na kufikia 75.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika Bajeti ya Mwaka 2021/2022, Serikali imepanga kuendelea kuboresha huduma ya maji safi na salama katika Mji wa Gairo ambapo kazi zitakazofanyika ni pamoja na ulazaji wa mabomba yenye urefu wa kilometa 21.8 ili kupeleka maji majumbani na ujenzi wa vituo vya kuchotea maji 40. Aidha, kwa lengo la kuongeza uzalishaji maji, Serikali imepanga kutekeleza Mradi wa Maji wa Chagongwe utakaonufaisha maeneo ya Mji wa Gairo na vijiji vya pembezoni.