Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 62 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Waziri wa Mifugo na Uvuvi 527 2021-06-30

Name

Seif Khamis Said Gulamali

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manonga

Primary Question

MHE. SEIF K. S. GULAMALI aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itatoa fedha za ujenzi wa majosho katika Wilaya ya Igunga, hususan Jimbo la Manonga?

Name

Abdallah Hamis Ulega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkuranga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Mifugo na Uvuvi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Seif Khamis Said Gulamali, Mbunge wa Manonga, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Halmashauri ya Igunga ina jumla ya majosho 20. Kati ya hayo majosho 12 yanafanyakazi na majosho nane ni mabovu na hayafanyi kazi na hivyo kuhitaji ukarabati.

Aidha, halmashauri hiyo inahitaji jumla ya majosho 36 na hivyo ina upungufu wa majosho mapya 16 yanayohitajika kujengwa. Kati ya majosho mabovu nane, majosho matatu yanakarabatiwa na josho jipya moja linajengwa na halmashauri yenyewe kwa kutumia vyanzo vyake vya fedha za ndani.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika Mwaka wa Fedha 2021/2022 jumla ya majosho 10 yatajengwa katika Halmashauri ya Igunga yakiwemo majosho matatu katika Jimbo la Manonga.

Mheshimiwa Naibu Spika, Ili kukabiliana na upungufu wa majosho, Halmashauri ya Igunga inashauriwa kuendelea kutenga asilimia 15 ya fedha inayokusanywa kutokana na mifugo kwa ajili ya kujenga na kukarabati majosho.