Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 62 Community Development, Gender and Children Wizari wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto 524 2021-06-30

Name

Husna Juma Sekiboko

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HUSNA J. SEKIBOKO aliuliza: -

Je, Serikali haioni umuhimu wa kuhamisha Dawati la Kijinsia kutoka Jeshi la Polisi na kwenda kwenye Vituo vya kutolea Huduma za Afya?

Name

Mwanaidi Ali Khamis

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Husna Sekiboko, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inaendeshwa kwa mujibu wa Sheria mbalimbali za Nchi. Jeshi la Polisi limepewa mamlaka kwa mujibu wa Sheria ya Jeshi la Polisi na Polisi Wasaidizi, Fungu Na. 5, Kifungu kidogo cha (322) ya mwaka 1965 na kuboreshwa mwaka 2002 ya kulinda raia na mali zake na kupeleleza makosa mbalimbali. Hivyo, Dawati hilo ni vyema likaendelea kukaa lilipo sasa badala ya kwenye vituo vya kutolea huduma ya afya.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika kuhakikisha kuwa waathirika wa vitendo vya ukatili wa kijinsia wanapatiwa huduma rafiki na za haraka, Dawati hili hushirikiana na Vituo vya Mkono kwa Mkono ambavyo viko kwenye Vituo vya Afya vikiwa na Wataalam wa Afya, Maafisa wa Jeshi la Polisi, Ustawi wa Jamii na Wanasheria kwa ajili ya utoaji wa huduma stahiki.