Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 3 Sitting 52 Defence and National Service Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga taifa 448 2016-06-28

Name

Hassan Elias Masala

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nachingwea

Primary Question

MHE. HASSAN E. MASALA aliuliza:-
Nachingwea ni miongoni mwa Wilaya chache zilizo na historia ndefu katika kusaidia nchi nyingi za Afrika kupata uhuru; kwani wapiganaji wengi wa nchi hizo walihifadhiwa kwenye Kambi ya Ukombozi Farm 17 iliyopo Nachingwea:-
(a) Je, Serikali ina mpango gani wa kuhifadhi na kuendeleza maeneo ya Kambi ya Farm 17 hata kama yamegeuzwa kuwa Sekondari ili kuwa maeneo ya kihistoria na kuweza kuwavutia watalii?
(b) Je, Serikali ina mpango gani wa kuzishawishi nchi zilizonufaika na Kambi ya Farm 17 kama Msumbiji na Zimbabwe ili ziangalie kwa karibu kambi hiyo kwa lengo la kuhifadhi kumbukumbu muhimu zilizopo?

Name

Dr. Hamisi Andrea Kigwangalla

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO – (K.n.y WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA) alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Hassan Elias Masala Mbunge wa Jimbo la Nachingwea kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kuwa Farm17 ni miongoni mwa maeneo yaliyotumiwa na wapigania uhuru wa nchi za Kusini mwa Afrika katika harakati za ukombozi. Serikali kwa kupitia Wizara ya Habari, Utamaduni, Michezo Sanaa na Vijana imeanzisha mradi ujulikanao kama Road to Independence kwa lengo la kutunza kumbukumbu za historia ya ukombozi wa Bara la Afrika ikiwemo Farm 17. Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa itashirikiana na Wizara hiyo katika kuhakikisha kuwa eneo hili linatunzwa ipasavyo ili kuvutia watalii wakaolitembelea. Aidha, tunapenda kuushauri uongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea kusaidia shule ya sekondari Farm 17 kuendeleza uhifadhi wa miundombinu ya kihistoria iliyopo shuleni hapo ili kutunza historia hiyo muhimu ya ukombozi.
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali haina mpango wa kuzishawishi nchi zilizopata hifadhi ya wapigania uhuru hapa nchini, kusaidia juhudi za uhifadhi wa maeneo hayo kwani nchi zenyewe zina hiari ya kuona umuhimu huo kwani lengo la Serikali ilikuwa ni kusaidia harakati za ukombozi kwa nchi husika.