Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 61 Finance and Planning Wizara ya Fedha na Mipango 518 2021-06-29

Name

Najma Murtaza Giga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NAJMA MURTAZA GIGA: aliuliza: -

Kumekuwa na kawaida kwa baadhi ya Taasisi za Serikali kutotumia huduma za Shirika la Bima la Zanzibar kwa kisingizio kuwa shirika hilo siyo la Umma.

(a) Je, Serikali inalitambua shirika hilo kama la Serikali au shirika binafsi?

(b) Kama ni shirika la Serikali, nini wito wa Serikali kwa watendaji ambao wamekuwa wakikataa kutumia huduma hiyo kwa kisingizio cha kuwa siyo shirika la Serikali?

Name

Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Magharibi

Answer

NAIBU WAZIRI OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA K.n.y. WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Fedha na Mipango, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Najma Murtaza Giga, Mbunge Viti Maalum lenye sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo: -

(a) Mheshimiwa Naibu Spika, Shirika la Bima la Zanzibar yaani Zanzibar Insurance Corporation limesajiliwa kwa mujibu wa Sheria ya Bima Namba 10 ya mwaka 2009 na lina leseni hai yenye usajili Na.00000704 inayoruhusu Shirika hilo kufanya biashara ya bima za kawaida yaani Non-Life Insurance. Shirika hilo linamilikiwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa asilimia 100. Hivyo, Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inatambua kuwa shirika hilo ni mali ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na sio Shirika binafsi.

(b) Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa Shirika la Bima la Zanzibar ni mali ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, wito wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa watendaji ambao wamekuwa wakikataa kutumia huduma zake kuendelea kulitumia shirika hilo kwa ajili ya kupata huduma za bima kama ambavyo wanalitumia Shirika la Bima la Taifa hasa ukizingatia kuwa biashara ya bima nchini ni biashara Huru na Huria inayosimamiwa na Sheria ya Bima Namba 10 ya mwaka 2009 pamoja na Kanuni zake. Ahsante. (Makofi)