Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 61 Industries and Trade Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara 516 2021-06-29

Name

Abubakar Damian Asenga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilombero

Primary Question

MHE. ABUBAKARI D. ASENGA aliuliza: -

Je, Serikali ina mikakati gani ya kuanza uzalishaji katika Kiwanda cha Chuma Mang’ula?

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Viwanda na Biashara naomba kujibu swali la Mheshimiwa Abubakari Damian Asenga, Mbunge wa Kilombero kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ujenzi wa uchumi wa viwanda hapa nchini, pamoja na mambo mengine unalenga kufufua na kuendeleza viwanda vilivyobinafsishwa ambavyo havifanyi kazi.

Mheshimiwa Naibu Spika, Mang’ula Mechanical Workshop ni karakana iliyoanzishwa kwa msaada wa Serikali ya China mwaka 1969. Karakana hiyo ilianzishwa kwa lengo la kurahisisha upatikanaji wa vipuri mbalimbali ya mitambo iliyokuwa inatumika wakati wa ujenzi wa Reli ya Tanzania-Zambia (TAZARA), pamoja na utengenezaji wa vipuri sehemu ya eneo la karakana hiyo ilitumika kujenga kiwanga cha Pre-Fabricated Concrete Manufacturing kwa ajili ya kutengeneza mataruma ya zege kwa maana ya concrete slippers na nguzo za zege.

Mheshimiwa Naibu Spika, karakana ya Mang’ula Mechanical and Machine Tools Company Limited ilirejeshwa Serikalini mwaka 2019 kutokana na mwekezaji wake kushindwa kuendeleza kiwanda hicho kwa mujibu wa mkataba wa mauziano. Kufuatia urejeshwaji huo Wizara ya Viwanda na Biashara na Ofisi ya Msajili wa Hazina imeandaa utaratibu wa kutafuta wawekezaji wapya watakaoviendesha viwanda hivyo kikiwemo kiwanda cha Mang’ula Machine and Mechanical Tools Limited.