Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 61 Water and Irrigation Wizara ya Maji 515 2021-06-29

Name

Venant Daud Protas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Igalula

Primary Question

MHE. VENANT D. PROTAS aliuliza: -

(a) Je, ni lini Serikali itakamilisha mradi wa kupeleka maji ya Ziwa Victoria katika Kata za Kigwa, Goweko, Igalula na Nsololo?

(b) Je, Serikali ina mpango gani wa uchimbaji wa mabwawa katika Kata za Mmale, Miswaki, Lutende na Kizengi ili kupunguza changamoto ya upatikanaji wa maji katika maeneo hayo?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Venant Daud Protas, Mbunge wa Igalula lenye sehemu (a) na (b) kwa pamoja kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, katika mwaka wa fedha 2021/2022, Serikali imepanga kuboresha huduma ya maji kwenye Kata za Kigwa, Goweko, Igalula na Nsololo kupitia bomba kuu linalotoa maji Ziwa Victoria kupeleka Miji ya Nzega, Igunga na Tabora.

Kazi zitakazofanyika ni pamoja na ujenzi wa tenki lenye ujazo wa lita 1,000,000 na ulazaji wa mabomba yenye urefu wa kilometa 122. Mradi huu unatarajiwa kukamilika kabla mwezi Juni, 2022 na utanufaisha wananchi wapatao 123,764 kwa kupata huduma ya maji safi, salama na yenye kutosheleza.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imepanga katika robo ya pili ya mwaka wa fedha 2021/2022 kukamilisha usanifu wa ujenzi wa bwawa katika Kata ya Kizengi na wakandarasi watapatikana mwezi Machi, 2022 kwa ajili ya ujenzi wa bwawa hilo ambapo wananchi wa Kata za Kizenga, Mmale, Miswaki na Lutende zaidi ya 60,000 watanufaika.