Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 61 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 514 2021-06-29

Name

Leah Jeremiah Komanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Meatu

Primary Question

MHE. LEAH J. KOMANYA aliuliza: -

Je, ni lini ujenzi kwa kiwango cha lami wa barabara ya Kolandoto – Oldean Junction utaanza kwa kuwa upembuzi yakinifu na usanifu wa kina ulishafanyika?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, ninaomba kujibu swali la Mheshimiwa Leah Jeremiah Komanya, Mbunge wa Meatu, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, barabara ya Kolandoto –Lalago – Mwanhuzi – Sibiti – Qangded – Oldean Junction yenye urefu wa kilometa 328 ni barabara kuu inayounganisha Mikoa ya Shinyanga, Simiyu, Singida na Arusha.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika mwaka wa fedha 2021/2022 Serikali imetenga kiasi cha shilingi milioni 2,000 kwa ajili ya kuanza ujenzi kwa awamu kwa kiwango cha lami kwa sehemu ya barabara ya Kolandoto – Mwanhuzi yenye urefu wa kilometa 62.5 na shilingi milioni 3,000 kwa ajili ya barabara ya Lalago – Ngóboko – Mwanhuzi yenye urefu wa kilometa 74 ambayo ni sehemu ya barabara aliyoitaja Mheshimiwa Mbunge. Ujenzi wa barabara hizi utaendelea kutekelezwa kulingana na upatikanaji wa fedha.

Mheshimiwa Naibu Spika, wakati juhudi za kuanza ujenzi wa barabara hizo zikiendelea, Serikali itaendelea kutenga fedha za matengenezo ya barabara hii ili iweze kupitika majira yote ya mwaka. Katika mwaka wa fedha 2021/2022 shilingi milioni 849.97 zimetengwa kwa sehemu ya Kolandoto hadi Mwangongo mkoani Shinyanga, shilingi milioni 540.995 zimetengwa kwa sehemu ya Mwangongo hadi Sibiti mkoani Simiyu, shilingi milioni 579.118 zimetengwa kwa sehemu ya Sibiti hadi Matala mkoani Singida na shilingi milioni 1,507.352 zimetengwa kwa sehemu ya Matala hadi Oldean mkoani Arusha. Ahsante.