Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 61 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 513 2021-06-29

Name

Simon Songe Lusengekile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busega

Primary Question

MHE. SIMON S. LUSENGEKILE aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara ya kutoka Nyashimo Wilayani Busega hadi Dutwa Wilayani Bariadi kupitia Shigala, Malili, Ngasamo na Imakanate yenye kilometa 47 kwa kiwango cha lami?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. MWITA M. WAITARA) alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, ninapenda kujibu swali la Mheshimiwa Simon Songe Lusengekile, Mbunge wa Busega, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Barabara ya Nyashimo –Dutwa ni barabara ya Mkoa yenye ureu wa kilometa 47 inayohudumiwa na Wizara yangu kupitia Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS).

Mheshimiwa Naibu Spika, barabara ya Nyashimo –Dutwa ipo katika mpango mkakati wa Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi (Ujenzi) kupitia Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) wa mwaka 2021/2022 – 2025/2026 kwa ajili ya kufanyiwa upembuzi yakinifu na usanifu wa kina. Barabara hii inaendelea kufanyiwa matengenezo mbalimbali pamoja na ujenzi wa madaraja ili iweze kupitika majira yote ya mwaka ambapo katika mwaka wa fedha 2021/2022 imetengewa shilingi milioni 1,102.607 kwa ajili ya matengenezo pamoja na ujenzi wa Daraja la Shigala na la Malili. Ahsante.