Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 61 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 510 2021-06-29

Name

Anna Richard Lupembe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nsimbo

Primary Question

MHE. ANNA R. LUPEMBE aliuliza: -

Barabara ya kutoka Ilembo hadi Itenka ni barabara muhimu kiuchumi.

Je, ni lini Serikali itaifanyia ukarabati barabara hii?

Je, ni lini sasa Serikali itaweka hela ya kutosha kuhakikisha barabara hii inakwisha kabisa kwa sasbabu ni barabara hii ya kiuchumi?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu la pili; kwa sababu kalvati kutokana na mvua nyingi zinazonyesha, makalvati haya yanachukuliwa hatimae inakuwa siyo barabara ya kalvati tena yanakuwa madaraja, na mpaka sasa hivi tunasema tumetengeneza makalvati matano, na najua si muda mrefu makalvati haya yatachukuliwa na mvua.

Je ni lini Serikali sasa itatenga pesa za kutengeneza madaraja, yapo makalvati matano sasa yatatengenezwa madaraja matano, ni lini Serikali itatoa pesa?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana, naomba kujibu maswali madogo mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Anna Richard Lupembe, Mbunge Jimbo la Nsimbo, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza alichokuwa anaomba kufahamu ni kwamba lini Serikali itatenga fedha za kutosha katika barabara hiyo ili kuhakikisha inakamilika?

Nimwambie tu kwamba Mheshimiwa Mbunge Serikali tutaendelea kuzingatia hilo ombi alilolisema lakini kwa kadri ya bajeti yetu inavyoendelea kuongezeka ndivyo tunavyoendelea kutenda fedha za kutosha kwa ajili ya barabara hiyo.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali lake la pili ilikuwa lini badala ya kujenga makalavati anataka tujenge madaraja katika eneo husika. Nimwambie tu kwamba sisi tunajenga kulingana na tathmini ambayo inafanywa na wakandarasi wa maeneo husika. Kwa hiyo, kama kutakuwa na hitaji la msingi la kujenga madaraja tutafanya hivyo baada ya kufanya na kupata tathmini ya kina katika barabara hiyo kuhusu hayo makalavati anayoyazungumzia Mheshimwa Mbunge, ahsante sana.

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, nimshukuru sana Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu mazuri, na nataka kumpongeza Mheshimiwa Anna Lupembe kwa swali lake zuri.

Mheshimiwa Naibu Spika, niwatoe hofu Waheshimiwa Wabunge, mpango wetu Ofisi ya Rais - TAMISEMI kwa mwaka 2022/2023 ni kujenga madaraja na makalvati yote, kwa hiyo, sasa hivi tumeshaelekeza TARURA katika Halmashauri zote kufanya usanifu, kazi inayofanyika sasa hivi ni usanifu wa madaraja na makalvati ili tuweze kujua gharama halisi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sababu tumeona tunaweze kutoa hela tukajenga barabara, lakini kama madaraja na makalvati hayajajengwa hayapitiki maana yake tumefanya kazi bure. Kwa hiyo kipaombele chetu sasa tunataka mwakani tukaelekeze kwenye madaraja na makalvati, kwa hiyo, niwatoe hofu tu waheshimiwa wabunge hili swala tumelipa kipaumbele. (Makofi)