Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 60 Energy and Minerals Wizara ya Nishat 505 2021-06-28

Name

Abeid Ighondo Ramadhani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Kaskazini

Primary Question

MHE. ABEID R. IGHONDO aliuliza: -

Je, ni lini Vijiji na Kata katika Jimbo la Singida Kaskazini ambavyo havijapata umeme vitapata umeme?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Nishati naomba kujibu swali la Mheshimiwa Abeid Ighondo Ramadhani, Mbunge wa Singida Kaskazini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, vijiji 26 vya Jimbo la Singida Kaskazini ambavyo havijapata umeme kati ya vijiji 84 vitapelekewa umeme kupitia utekelezaji wa Mradi wa REA Awamu ya Tatu Mzunguko wa Pili ulioanza mwezi Machi, 2021. Utekelezaji wa mradi huu unatarajiwa kukamilika ifikapo mwezi Desemba, 2021 na gharama ya mradi ni shilingi bilioni 26.6.