Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 60 Water and Irrigation Wizara ya Maji 502 2021-06-28

Name

Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Primary Question

MHE. JAPHET N. HASUNGA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itamaliza tatizo la maji katika Mji wa Vwawa?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Japhet Ngailonga Hasunga, Mbunge wa Vwawa kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, mahitaji ya maji ya Mji Vwawa ni zaidi ya lita milioni 10 kwa siku ambapo kwa sasa hali ya upatikanaji wa huduma ya maji ni asilimia 43.2.

Mheshimiwa Spika, Serikali inatekeleza mipango ya muda mfupi na muda mrefu ili kuboresha huduma ya maji safi na salama katika Mji wa Vwawa ambapo katika mpango wa muda mfupi mwaka 2020/2021, Wizara imechimba visima virefu vitatu vyenye uwezo wa kuzalisha maji lita 600,000 kwa siku. Ujenzi wa miundombinu ya usambazaji maji ya visima hivyo utafanyika ndani ya mwaka wa fedha 2021/2022 na kuongeza huduma ya upatikanaji wa maji kwa wakazi wa Mji wa Vwawa kufikia asilimia 70.

Mheshimiwa Spika, katika mpango wa muda mrefu wa kuboresha huduma maji safi, salama na yenye kutosheleza kwa wakati wa mji huo Serikali imepanga kujenga mradi kupitia chanzo cha maji cha Mto Bupigu uliopo Wilaya ya Ileje wenye uwezo wa kuzalisha maji kiasi cha lita milioni 73 kwa siku. Mtaalam Mshauri kwa ajili ya kufanya Usanifu wa Kina yaani detailed design wa mradi huu anatarajiwa kupatikana katika robo ya kwanza ya mwaka 2021/2022 mradi huu utanufaisha Miji ya Vwawa, Mlowo na Tunduma katika Mkoa wa Songwe.