Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 2 sitting 3 Natural Resources and Tourism Wizara ya Maliasili na Utalii 36 2016-01-28

Name

Cecilia Daniel Paresso

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. CECILIA D. PARESSO aliuliza:-
Katika Bunge la Kumi aliyekuwa Waziri wa Maliasili na Utalii aliunda Kamati Ndogo ya kushughulikia mgogoro uliopo kati ya wananchi wa Kata ya Buger na Hifadhi ya Taifa ya Manyara:-
(a) Je, ni nini matokeo ya Kamati Ndogo iliyoundwa?
(b) Je, ni lini wananchi watapewa taarifa ya Kamati Ndogo iliyokuwa inashughulikia mgogoro huo?

Name

Eng. Ramo Matala Makani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Cecilia Daniel Paresso, lenye sehemu (a) na (b) kwa pamoja, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Waziri wa Maliasili na Utalii alifanya ziara katika Wilaya ya Karatu tarehe 2 Juni, 2015 na kuteua Tume iliyopewa Hadidu za Rejea kuhusu kutatua mgogoro baina ya wananchi wa Kata ya Buger na Hifadhi ya Taifa ya Manyara.
Tume ilifanya mahojiano na makundi mbalimbali na kupitia taarifa zote zilizotolewa na Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) na Taarifa ya awali imeandaliwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, Taarifa ya Tume imebaini kuwa kwa ujumla chanzo kikubwa cha migogoro baina ya wananchi na Hifadhi ya Taifa ya Ziwa Manyara ni idadi kubwa ya mifugo na kukosekana eneo la kuchungia katika Kijiji cha Buger. Tume imependekeza hatua za kuchukuliwa ambazo ni pamoja na hizi zifuatazo:-
(a) Kufanya sensa ya mifugo kwa vijiji vilivyopo katika Kata ya Buger ili kubaini idadi ya mifugo iliyopo dhidi ya ukubwa wa ardhi waliyonayo;
(b) Vijiji kuandaa mpango wa matumizi bora ya ardhi;
(c) Kutoa elimu ya uhifadhi na Sheria katika vijiji vinavyozunguka hifadhi, hasa Msitu wa Marang;
(d) Kuanzisha Kamati za Mazingira za Vijiji na kuimarisha zilizopo ili kutekeleza vema majukumu yake; na
(e) TANAPA kuweka nguvu katika kuchangia miradi ya maendeleo ya jamii kwenye vijiji vinavyozunguka hifadhi.
Mheshimiwa Naibu Spika, Wizara itaandaa kikao cha wadau ndani ya miezi mitatu ili kuwasilisha mapendekezo ya Kamati na kujadili utekelezaji wake.