Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 58 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 485 2021-06-24

Name

Cecil David Mwambe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ndanda

Primary Question

MHE. CECIL D. MWAMBE aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itasaidia na kufanikisha kutoa Namba kwa Vijiji vya Chipunda, Mkalinda na Sululu ya Leo vyenye wakazi zaidi ya elfu kumi katika Jimbo la Ndanda?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE) alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Cecil David Mwambe, Mbunge wa Jimbo la Ndanda, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Vijiji vya Chipunda na Sululu ni vijiji halali ambavyo vimeendelea pia kutambulika kupitia Matangazo ya Serikali Namba 536 Mamlaka za Miji na 537 Mamlaka za Wilaya ya tarehe 19/07/2019. Vijiji hivyo pia vilishiriki kikamilifu katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa uliofanyika mwaka 2019.

Mheshimiwa Naibu Spika, kutokana na changamoto ya uchakavu na upotevu wa Hati za Usajili za baadhi ya Vijiji, mwaka 2019/2020, Ofisi ya Rais – TAMISEMI ilihuisha taarifa za vijiji vyote nchini na kuandaa kanzidata ya Hati za Usajili wa Vijiji vyote nchini kwa kuzingatia matakwa ya kifungu cha 22 na 26 cha Sheria ya Serikali za Mitaa, Mamlaka za Wilaya, Sura ya 287. Hati hizo kwa sasa zipo katika hatua ya uchapishaji na zitatolewa kwa vijiji vyote nchini.

Mheshimiwa Naibu Spika, kutokana na zoezi hilo, Kijiji cha Chipunda kilichopo Kata ya Mkululu, Halmashauri ya Wilaya ya Masasi Namba yake ya Usajili ni MTR-091-0900989. Kijiji cha Sululu kilichopo Kata ya Sululu, Halmashauri ya Mji wa Masasi Namba yake ya Usajili ni MTR-092-09011574.Kijiji cha Mkalinda hakipo katika Orodha ya Vijiji vilivyopo nchini.