Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 57 Industries and Trade Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara 479 2021-06-23

Name

Eng. Ezra John Chiwelesa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Biharamulo Magharibi

Primary Question

MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa Soko la Kimkakati la Rusahunga Wilayani Biharamulo litakalogharimu shilingi bilioni 3.5 kama alivyoeleza Mheshimiwa Waziri Mkuu Bungeni?

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Viwanda na Biashara, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Engineer Ezra John Chiwelesa, Mbunge wa Biharamulo Magharibi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inatambua umuhimu wa kuwa na masoko nchini kwa ajili ya kukuza biashara na mauzo ndani na nje ya nchi kwa maendeleo na ustawi wa wananchi wake. Kutokana na umuhimu huo, Serikali imekuwa ikichukua hatua mbalimbali za kuhakikisha masoko yanaanzishwa, kuboreshwa na kuendelezwa ili kutoa fursa kwa wakulima wadogo pamoja na wafanyabishara kuuza mazao na bidhaa zao katika masoko hayo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali katika kipindi cha mwaka 2017/2018, Halmashauri ya Wilaya ya Biharamulo ilitenga eneo la uwekezaji katika Kata ya Lusahunga lenye ukubwa wa ekari 65 ambalo lina thamani ya shilingi bilioni 3.5. Eneo hili limetengwa kwa ajili ya kujenga viwanda vya kusindika mazao ya kilimo, kujenga maghala ya kuhifadhia mazao, miundombinu ya majengo ya kibiashara kama mahoteli, ujenzi wa soko la kimkakati, kituo cha afya, viwanja vya makazi, na kituo cha mafunzo ya wakulima.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kupitia Programu ya Kuendeleza Sekta ya Kilimo Awamu ya Pili (ASDP II) imeendelea kusisitiza Halmashauri ya Wilaya ya Biharamulo kutenga fedha katika bajeti yake ili kufanikisha ujenzi wa soko hilo. Aidha, Serikali inaendelea kutafuta wadau mbalimbali ikiwemo Mifuko ya Hifadhi ya Jamii ili iweze kufanikisha ujenzi wa soko hilo.