Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 57 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 478 2021-06-23

Name

Dr. Alice Karungi Kaijage

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. ALICE K. KAIJAGE aliuliza: -

Je, Serikali imejipangaje kutatua changamoto iliyopo katika vituo vya kutolea huduma za afya ya kukosekana kwa Idara ya Huduma ya Mazoezi Tiba na Utengamao ukilinganisha na ongezeko la wagonjwa wanaohitaji aina hiyo ya tiba?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Alice Karungi Kaijage, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kuwa kuna ongezeko kubwa la uhitaji wa huduma ya mazoezi tiba na utengamao kwenye vituo vya kutolea huduma za afya, huku kukiwa na changamoto ya uwepo wa miundombinu stahiki, vifaa na wataalam kwenye vituo vingi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto imefanya tathmini ya mahitaji wa huduma ya mazoezi tiba na utengamao kwenye vituo vya kutolea huduma za afya na inaendelea kukamilisha mpango mkakati ambao utatoa mwongozo katika kutatua uhitaji wa huduma hizo. Ofisi ya Rais, TAMISEMI itatekeleza kikamilifu mpango utakaotolewa ili kuboresha huduma ya mazoezi tiba na utengamao katika vituo vya afya. Ahsante.