Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 56 Works, Transport and Communication Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari 474 2021-06-22

Name

Jackson Gedion Kiswaga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalenga

Primary Question

MHE. JACKSON G. KISWAGA aliuliza: -

Je, Serikali haioni uamuzi wa kutaka ifikapo tarehe 1 Mei, 2021 wasajili wa namba za simu za mkononi mitaani (freelancers) wawe katika maduka unaweza kufuta ajira zaidi ya 40,000 na kudhoofisha lengo lake la ajira milioni nane ifikapo mwaka 2025?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari naomba kujibu swali la Mheshimiwa Jackson Gedion Kiswaga, Mbunge wa Kalanga kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli tarehe 16 Februari, 2021 Serikali kupitia Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) iliwaelekeza watoa huduma kutekeleza takwa la kikanuni la usajili wa laini za simu kibayometria kwa kuwatumia mawakala wanaokidhi vigezo kwa mujibu wa Kanuni ya 10 ya Kanuni za Usajili wa Laini za Simu ya 2020 (The Electronic and Postal Communications (SIM Card Registration) Regulations, 2020 GN No. 112 ya 2020.

Mheshimiwa Spika, kutokana na umuhimu wa freelancers kwenye sekta, kiuchumi na katika kulinda ajira zao, tarehe 14 Aprili, 2021 Serikali ilisitisha zuio kwa watoa huduma kutowatumia freelancers katika usajili wa laini za simu kibayometria, kwa kutoa taarifa kwa umma na kwa kuwaandikia watoa huduma barua ya kuondoa zuio hilo.

Mheshimiwa Spika, Serikali kwa kushirikiana na watoa huduma imetengeneza rasimu ya mwongozo wa kuwatambua na kuratibu kazi za freelancers ili kuondoa mapungufu yaliyojitokeza na kuweka bayana uhusiano kati ya watoa huduma na freelancers, ahsante.