Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 56 Natural Resources and Tourism Wizara ya Maliasili na Utalii 472 2021-06-22

Name

Cecilia Daniel Paresso

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. CECILIA D. PARESSO aliuliza: -

Je, nini kauli ya Serikali kuhusiana na baadhi ya askari wa TANAPA wanaolinda Hifadhi ya Msitu wa Marang inayopakana na Kata ya Buger Wilayani Karatu kujichukulia sheria mkononi na kuwaua wananchi wanaoingia kwenye hifadhi?

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Cecilia Daniel Paresso, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, baadhi ya wananchi wanaozunguka Hifadhi ya Msitu wa Marang, hasa wafugaji wanapoingiza mifugo yao hifadhini na kukamatwa na askari wa hifadhi, hukataa kutii sheria bila shuruti na kupiga yowe maalum ijulikanayo kama HAYODAA ikiwa ni kiashiria cha hatari kwa kabila la Wairaki. Hivyo, wananchi wengi hujitokeza wakiwa na silaha za jadi zikiwemo fimbo, mishale, mapanga na mikuki ili kuwadhuru askari wa hifadhi na kupinga ukamataji huo wa mifugo na kuchukua mifugo yao kwa kutumia nguvu.

Mheshimiwa Spika, yamefanyika matukio mengi ya askari kunyang’anywa silaha au mifugo iliyokamatwa hifadhini na wananchi ambapo husababisha kutokuelewana kati ya askari wa hifadhi na wananchi. Kati ya mwaka 2013 hadi 2020 jumla ya matukio saba yalitokea ambayo yalihusisha wananchi kuwashambulia askari wa hifadhi, kuwajeruhi na wengine kupoteza maisha.

Mheshimiwa Spika, Serikali kwa kushirikiana na wadau pamoja na wananchi wa maeneo hayo imeandaa Mpango wa Matumizi ya Ardhi ambapo kwa sasa hati zinaandaliwa na baada ya uhakiki wananchi watakabidhiwa hati hizo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha.