Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 54 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 447 2021-06-18

Name

Grace Victor Tendega

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA K.n.y. MHE. GRACE V. TENDEGA aliuliza: -

Suala la Vitambulisho vya ujasiriamali limekuwa ni changamoto hasa kwa Wafanyabiashara ambao wana mitaji midogo.

Je, Serikali ina mkakati gani wa kuboresha au kufuta vitambulisho hivyo?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE) alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, ofisi ya Rais TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Grace Victor Tendega, Mbunge viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwezi Machi 2019, Serikali kwa kuwathamini na kuwajali wajasiriamali na watoa huduma wadogo ilianzisha utaratibu wa vitambulisho ili kuwawezesha kufanya biashara katika mazingira bora na tulivu zaidi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kwamba kweli kuna changamoto zilizojitokeza katika utoaji wa vitambulisho kwa wajasiriamali na watoa huduma wadogo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Ofisi ya Rais -TAMISEMI imefanya tathmini ya zoezi zima la ugawaji, usajili na matumizi ya vitambulisho vya wwajasiriamali na watoa huduma wadogo katika mikoa na halmashauri ili kubaini changamoto zilizopo na kufanya maboresho.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuanzia mwaka 2021 vitambulisho hivyo vimefanyiwa maboresho kadhaa ikiwemo kuwekwa picha na jina la mjasiriamali mdogo aliyepatiwa kitambulisho pamoja na ukomo wa muda wa kutumika kitambulisho hicho ambao ni mwaka mmoja tangu tarehe ya kupatiwa kitambulisho badala ya mwaka wa kalenda kama ilivyokuwa awali.