Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 53 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 441 2021-06-17

Name

Omari Mohamed Kigua

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilindi

Primary Question

MHE. OMARI M. KIGUA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itajenga daraja linalounganisha Wilaya ya Kilindi na Kiteto kupitia Kijiji cha Sambu?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA ZIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE) alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais - TAMISEMI naomba kujibu swali la Mheshimiwa Omari Mohamed Kigua, Mbunge wa Kilindi kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, barabara ya Mnadani – Sambu - Pagwi ni barabara ya mkusanyo (Collector Road) yenye urefu wa kilomita 38. Barabara hii inaanzia barabara ya TANROADS ya Kwaluguru-Songe-Kibirashi inapita katika maeneo ya Changanyikeni, Kigunga, Sambu, Makelele, Lumotio, Pagwi na kuishia katika eneo la Lugira katika Wilaya ya Kiteto ambako inaungana na barabara ya Kijungu – Sunya – Dongo katika Mkoa wa Manyara.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika mpango na bajeti ya mwaka wa fedha 2021/2022 barabara hii imetengewa kiasi cha shilingi milioni 182.52 kupitia fedha za Mfuko wa Barabara (Road Fund) kwa ajili ya kufanya matengenezo ya barabara yenye urefu wa kilomita 10.5, ujenzi wa kalvati tisa na vivuko mfuto (drift)vinne.

Mheshimiwa Spika, barabara hii itaendelea kutengewa fedha kulingana na upatikanaji wa fedha kila mwaka ili kutatua changamoto iliyopo ya kutopitika kwa barabara hii.