Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 50 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 419 2021-06-14

Name

Martha Festo Mariki

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MARTHA F. MARIKI aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itakamilisha zoezi la utoaji wa Vitambulisho vya Taifa kwa wananchi kwa kuwa kumekuwa na changamoto ya upatikanaji wa vitambulisho hivyo?

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi naomba kujibu swali la Mheshimiwa Martha Festo Mariki Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kupitia Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa inaendelea kutekeleza mpango kazi wa kuzalisha vitambulisho, na inatarajiwa ifikapo Agosti, 2021 wananchi wote waliotambuliwa na kupewa namba za usajili watakuwa wamepatiwa vitambulisho. Aidha, mpango huu unalenga kuzalisha vitambulisho kwa awamu kwa kila wilaya, ambapo kwa kipindi cha kuanzia tarehe 14 Januari 2021 hadi kufikia tarehe 31 Mei, 2021 Mamlaka imefanikiwa kuzalisha na kusambaza vitambulisho 7,148,971 katika wilaya 73 nchini. Tanzania bara wilaya 63 na Zanzibar wilaya 10, na kazi ya uzalishaji inaendelea.

Mheshimiwa Naibu Spika, hadi kufikia mwezi Mei, 2021 Mamlaka imefanikiwa kugawa namba za utambulisho kwa wananchi 11,737,021 Kutokana na mfumo wa NIDA kuunganishwa na mifumo mingine ya taasisi za Serikali na binafsi. Aidha, wananchi wanaendelea kupata huduma mbalimbali za kijamii na kiuchumi kama vile huduma za kifedha, kufungua biashara, kupata namba ya mlipa kodi (TIN), kupata hati za kusafiria, umilikishaji ardhi na kusajili laini za simu kwa kutumia namba za utambulisho wakati wakisubiri kupatiwa vitambulisho vyao vya taifa. Nakushukuru.