Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 50 Education, Science,Technology and Vocational Training, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia 418 2021-06-14

Name

Dr. Thea Medard Ntara

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. THEA M. NTARA aliuliza:-

Je, Serikali ina mkakati gani wa kusomesha Wahadhiri wengi zaidi katika ngazi ya Shahada ya Uzamivu (Ph.D) kwani waliopo sasa ni wachache?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Thea Medard Ntara, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inao mpango mkakati wa kuongeza rasilimaliwatu katika taasisi za elimu ya juu ikijumuisha wahadhiri, wakutubi na wataalamu wa maabara na karakana ili kukidhi mahitaji ya viwango na ubora wa Elimu.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuanzia mwezi Julai, 2021 Serikali kupitia mradi wa Higher Education for Economic Transformation (HEET) ina mpango wa kusomesha jumla ya wahadhiri 430 katika kipindi cha miaka mitano (2021-2026) ili kukabiliana na upungufu huu katika fani za kipaumbele (Priority Programs) katika vyuo vikuu vya Serikali nchini.

Mheshimiwa Naibu Spika, sambamba na mpango huo mahsusi, vyuo vikuu navyo vinaendelea kusomesha wahadhiri wao kupitia vyanzo vingine, ikiwemo mikataba ya kitaalam ya utafiti (collaborative research projects) na scholarship mbalimbali tunazopokea kutoka nchi rafiki ambapo wahadhiri hupewa kipaumbele.

Mheshimiwa Naibu Spika, kupitia mipango hiyo, Jumla ya wahadhiri 621 katika ngazi ya shahada ya Uzamivu (PhD) na 241 katika Shahada ya Umahiri wanaendelea na masomo. Aidha kwa mwaka wa masomo 2021/2022 jumla ya wahadhiri 48 wanaendelea na masomo katika nchi mbalimbali. Kwa mfano katika nchi ya China wapo wanafunzi au wahadhiri 30, Uingereza 12 na Hangaria wahadhiri sita. Ahsante sana.