Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 50 Water and Irrigation Wizara ya Maji 415 2021-06-14

Name

Vincent Paul Mbogo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkasi Kusini

Primary Question

MHE. VINCENT P. MBOGO aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itatekeleza mradi wa maji wa Mji Mdogo wa Chala ambayo ni ahadi ya Mheshimiwa Rais wakati wa kampeni za mwaka 2020?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI K.n.y. WAZIRI WA MAJI alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Maji naomba kujibu swali la Mheshimiwa Vicent Paul Mbogo Mbunge wa Nkasi Kusini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Mji mdogo wa Chala unapata maji kutoka Mto Kauzike na Bwawa la Ntanganyika na hali ya upatikanaji wa huduma ya maji safi na salama katika Mji huo ni asilimia 56. Aidha, katika kuhakikisha huduma ya maji katika mji wa Chala inaboreshwa mwaka 2020/2021 ulitekelezwa mradi wa maji ambao umehusisha kuchimba kisima kirefu chenye uwezo wa kuzalisha lita 153,600 kwa siku na kiasi hiki kimeongeza upatikanaji wa maji zaidi ya lita 300,000 kwa siku. Hivyo kazi itakayofanyika kuanzia mwezi Julai, 2021 ni ujenzi wa miundombinu ya usambazaji maji, ujenzi wa nyumba ya mtambo wa maji, ufungaji wa pampu na ulazaji wa bomba mita 500 kwenda kwenye tanki lililopo la lita 150,000.

Mheshimiwa Naibu Spika, lengo la Serikali ni kuhakikisha wananchi wanapata huduma ya maji wakati wote, hivyo mpango wa muda mrefu katika mji wa Chala ni kutumia mabwawa madogo na ya ukubwa wa kati ambapo kwa sasa utafiti wa kubainisha maeneo yanayofaa kwa ajili ya ujenzi wa mabwawa mawili (2) katika Mji Mdogo wa Chala unaendelea na unatarajiwa kukamilika robo ya kwanza ya mwaka wa fedha 2021/2022.