Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 49 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Waziri wa Mifugo na Uvuvi 407 2021-06-10

Name

Yahya Ally Mhata

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nanyumbu

Primary Question

MHE. YAHYA A. MHATA aliuliza:-

Je, wananchi wa Jimbo la Nanyumbu watanufaika vipi na Shamba la Uzalishaji Mifugo Nangaramo?

Name

Abdallah Hamis Ulega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkuranga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mifugo na Uvuvi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Ally Yahya Mhata, Mbunge wa Nanyumbu kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Shamba la Nangaramo ni miongoni mwa mashamba matano ya kuzalisha mitamba chotara wa maziwa na nyama kwa lengo la kusambaza kwa wafugaji.

Mheshimiwa Spika, faida zinazopatikana kwa wananchi wanaozunguka Shamba la Nangaramo ni pamoja na wananchi kupata elimu kupitia mikutano ya ujirani mwema kuhusu fursa za upatikanaji wa mitamba ya maziwa na nyama kwa lengo la kuwahamasisha kufuga ili kuboresha lishe ya familia, kutoa ajira na mbolea kwa uzalishaji wa mazao.

Mheshimiwa Spika, mbili, kutoa mafunzo ya ufugaji bora kwa shule za msingi na sekondari. Aidha, wanafunzi kutoka katika Shule ya Sekondari Mkangaula wamenufaika na mafunzo hayo walipokuwa kwenye mafunzo maalum; na tatu, uongozi wa shamba hushiriki shughuli mbalimbali za kijamii kama vile ujenzi wa shule na utoaji wa ajira za muda mfupi na mrefu kwa wananchi.