Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 48 Industries and Trade Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara 404 2021-06-09

Name

Kenneth Ernest Nollo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bahi

Primary Question

MHE. KENNETH E. NOLLO aliuliza:-

Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga Kiwanda cha Chumvi katika Kata ya Ilindi, Wilayani Bahi kitakachosaidia kuongeza mapato ya Halmashauri ya Wilaya ya Bahi na kutoa ajira kwa wananchi hasa akina mama?

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA alijibu:-Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Viwanda na Biashara naomba kujibu swali la Mheshimiwa Kenneth Ernest Nollo, Mbunge wa Bahi kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, moja ya vipaumbele vya Serikali katika kipindi hiki ni kuhamasisha ujenzi na kuendeleza viwanda vinavyoongeza thamani ya rasilimali zinazopatikana kwa wingi nchini ikiwemo madini ya chumvi inayopatikana katika Kata za Ilindi na Chali katika Wilaya ya Bahi ili kukuza uchumi na kuongeza ajira.

Mheshimiwa Naibu Spika, takwimu zilizopo zinaonesha kuwa, shughuli za uchimbaji na ukusanyaji wa chumvi Wilayani Bahi, zimeajiri takribani watu 400 hasa vijana na akinamama. Serikali inafanya utafiti wa kujua kiasi cha chumvi kilichopo yaani salt deposit ili utafiti huo ukikamilika utumike katika kuhamasisha wawekezaji katika viwanda vya chumvi kwa kushirikiana na wadau mbalimbali ikiwemo Waheshimiwa Wabunge.

Mheshimiwa Naibu Spika, Wizara inashirikiana na Wizara nyingine za kisekta ikiwemo Wizara ya Maji ili kuhakikisha upatikanaji wa maji ya uhakika katika eneo hilo na Wizara ya Madini kujua kiasi cha madini ya chumvi kilichopo yaani salt deposit ili kuona kama kitakidhi kiwango cha uzalishaji kinachotakiwa kuendesha na kiwanda hasa kiwanda vya kati.

Mheshimiwa Spika, aidha, Serikali kupitia Shirika la Kuhudumia Viwanda Vidogo (SIDO) inafanya utafiti wa teknolojia rafiki ya kuwasaidia wajasiliamali wadogo ili kuzalisha chumvi kwa tija katika eneo la Ilindi, Bahi.