Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 47 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Wizara ya Kilimo 390 2021-06-08

Name

Eng. Stella Martin Manyanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nyasa

Primary Question

MHE. JOSEPH K. MHAGAMA K.n.y. MHE. ENG.STELLA M. MANYANYA aliuliza:-

Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha Bonde la Mto Ruhuhu lililopo Kata ya Lituhi linawanufaisha wananchi kwa kuweka miundombinu ya Kilimo na umwagiliaji?

Name

Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Kilimo, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Engineer Stella Martin Manyanya, Mbunge wa Jimbo la Nyasa kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua umuhimu wa Bonde la Mto Ruhuhu linalojumuisha sehemu ya Wilaya Ludewa Mkoni Njombe na Wilaya ya Nyasa Mkoani Ruvuma linalotumika kwa kilimo cha umwagiliaji. Upembuzi yakinifu wa awali kuhusu kilimo cha umwagiliaji katika bonde hili ulifanyika mwaka 2013/2014 na kubaini uwezekano wa kujenga bwawa kubwa; matumizi mbalimbali ikiwemo kilimo cha umwagiliaji kwa takribani hekta 4,000 na kufua umeme wa megawati 300. Tume ya Taifa ya Umwagiliaji kwa kushirikiana na Shirika la Umeme Tanzania linaendelea na upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa Bwawa la Kikonge lililopo ndani ya Bonde la Mto Ruhuhu kwa ajili ya uzalishaji wa umeme na uendelezaji wa miundombinu ya kilimo cha umwagiliaji chini ya Bwawa la Kikonge.

Mheshimiwa Spika, mara baada ya kazi ya upembuzi yakinifu na usanifu itakapokamilika na kutathimini gharama halisi, Serikali itatafuta fedha za ujenzi wa bwawa hili pamoja na fedha za ujenzi wa miundombinu ya umwagiliaji chini ya Bwawa la Kikonge ili kuongeza uzalishaji na tija ya mazao ya kilimo katika eneo hilo. (Makofi)