Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 47 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 388 2021-06-08

Name

Mwantum Dau Haji

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. STANSLAUS H. NYONGO K.n.y. MHE. MWANTUMU DAU HAJI aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itaanza kutoa elimu ya ujasiriamali kwa wanawake na vijana katika Halmashauri wanapewa mikopo ya asilimia tano?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais - TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mwantumu Dau Haji, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mujibu wa Kanuni ya 23 ya Kanuni za Utoaji na Usimamizi wa Mikopo ya asimilia 10 kwa Wanawake, Vijana na Watu wenye Ulemavu za mwaka 2019, Mamlaka za Serikali za Mitaa zinapaswa kutoa mafunzo kwa vikundi vilivyokubaliwa kupata mikopo hiyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuzingatia Kanuni hiyo Serikali ilikwishaanza kutoa elimu ya ujasiriamali na katika mwaka wa fedha 2019/2020 Mamlaka za Serikali za Mitaa zimetoa mafunzo kwa vikundi 11,915 vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu ambavyo vilipewa mikopo inayotokana na asilimia 10 ya mapato ya ndani ya Halmashauri zote nchini. Mafunzo yaliyotolewa ni pamoja na mafunzo ya ujasiriamali, utunzaji fedha, uendeshaji na usimamizi wa miradi, utoaji taarifa na usimamizi wa marejesho ya mikopo. Serikali kupitia Mamlaka za Serikali za Mitaa itaendelea kutoa elimu kwa vikundi hivyo ili kuvijengea uwezo wa kuendelea kukua na kutumia ipasavyo fursa mbalimbali za kiuchumi katika maeneo yao, ahsante.